MAKAMU MWENYEKITI UTEGA AONJA JOTO YA JIWE,ATIMULIWA MKUTANONI.

MAKAMU MWENYEKITI UTEGA AONJA JOTO YA JIWE,ATIMULIWA MKUTANONI.

   (MBUNGE WA JIMBO LA BUMBULI JANUARI MAKAMBA|}
 
NA RAISA SAID,BUMBULI.
Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Wakulima wa Chai{UTEGA} katika Halmashauri ya Wilaya ya Bumbuli Richard Mbuguni alipata wakati mgumu baada ya wakulima wa zao la chai kumtaka aondoke  katika mkutano wa hadhara uliofanyika mwishoni mwa juma kwa  kile  kilichoelezwa  kukosa  imani nae.
Uamuzi huo  wa wakulima  ulikuja baada  ya wao kuona hakuna  haja  ya  makamu mwenyekiti  huyo   kuendelea  kushiriki  kikao hicho  huku  wakidai  ni  mmoja  wa wasaliti  wa zao  hilo na ambao  wako upande  wa mwekezaji  ambaye  alikuwa  akiwanyanyasa  wakati wote licha  ya wao kuwaweka  madarakani  viongozi  hao.
Wakizungumza  kwa  nyakati  tofauti  wakulima  hao  wapatao  zaidi  ya 1000  ambao  walionekana  kuwa  na  jazba,  walisema  hawawezi kushirikiana  na  mtu  ambaye  anawanyonya    na  anayesabisha  uchumi  wa  Bumbuli   kushuka  kwa  kuendelea  kumkumbatia  muwekezaji  na  kuwasaliti wao ambao  ndio  wamiliki wa  kiwanda hicho.
Mmoja  wa  wakulima hao  alietambulika  kwa jina  la  Mustafa Soa,  mkazi  wa  kijiji  cha  Kweminyasa   alisema  wao kama  wakulima  hawezi  kujadili  mambo  yao  wakati   viongozi wa Chama  cha Utega  wakiendelea  kuwepo  katika  maeneo  ya mkutano   kwa kuwa  wao  tangu  zamani  hawako  pamoja nao.
Awali  ofisa  Tarafa  wa  Bumbuli  Ismail  Kimweri   katika  kuwatuliza  wakulima  hao  ili  wamuache  makamu  mwenyekiti  ashiriki  mkutano  huo alifikia  hatua  ya  kuwaimbia  wimbo  kwa lugha ya  kisambaa  wenye  maneno  “ Mkazio Kuhembezana wenye  maana  ya  unyumba  ni  mapatano  ambao  uligonga  mwamba.
Akizungumza  katika  mkutano huo wa kujadili uuzaji wa  majani  ya  chai  nje ya kiwanda cha Mponde, ambacho kwa sasa kimefungwa,  Mbunge  wa  Jimbo  la  Bumbuli  January  Makamba  aliwasihi  kuwa  wavumilivu  katika  kipindi  hiki cha mpito na kuwataka  waendelee kutunza zao la chai  na  wauze  majani  ya  chai  kwenye  viwanda  vingine vya  jirani ili waweze kujikimu  kimaisha.
Makamba  ambaye pia ni  Naibu  Waziri  wa  Mawasiliano  Sayansi  na  Teknolojia, alisema  amekwisha zungumza na menejimenti za viwanda hivyo ili viongeze uzalishaji na vifaa vya kusafirishia chai kutoka mashambani hadi kwenye viwanda.
Hata  hivyo  mbunge huyo  aliwataka   wakulima  hao  kuendelea kuwa  na subira  kwa kuwa  ufumbuzi  wa  kufunguliwa  kwa  kiwanda  hicho  unakaribia  kufikia  ukingoni  kwa kuwa  suala  hilo  liko  mikononi  mwa  ngazi  za  juu za  serikali.
Share this article :

Post a Comment

 
Copyright © 2011. TANGA LEO - All Rights Reserved
Proudly powered by Blogger