Yanga yapaa kileleni mwa Ligi Kuu.


Yanga yapaa kileleni mwa Ligi Kuu. 
 
 yangaaa

Ligi kuu ya soka nchini Tanzania bara imeendelea hii leo kwa mchezo mmoja uliopigwa kwenye uwanja wa taifa jijini Dar es salaam ukiwakutanisha Wenyeji Yanga na Mtibwa Sugar toka Morogoro .
Katika mchezo huo Yanga waliibuka na ushindi wa mabao mawili bila katika mchezo ambao walitawala kuanzia mwanzo hadi mwisho na wangeweza kushinda kwa idadi kubwa ya mabao .
Yanga walifunga mabao yote mawili kupitia kwa Kiungo mshambuliaji  Mrisho Khalfan Ngassa ambaye alifunga mabao mawili baada ya kuingia kipindi cha pili kuchukua nafasi ya mshambuliaji raia wa Liberia Kper Sherman .
Huu unakuwa ushindi wa pili mfululizo kwa Yanga baada ya kushinda mchezo wao dhidi ya Coastal Union kwa bao moja .
Matokeo haya yanawafanya yanga wapande  kwenye kilele cha ligi kuu ya Tanzania bara wakiwa na idadi ya pointi 25 wakiwazidi mabingwa watetezi Azam Fc kwa pointi tatu .
Share this article :

Post a Comment

 
Copyright © 2011. TANGA LEO - All Rights Reserved
Proudly powered by Blogger